|
1050.
Occurrence given to Raymond Aguilera on 16 May 1997. From Prophecy #1046 Reymundo, I want you to go to Mt. Shasta and make Three Stone Altars. One to the north, one to the east, and one to the south. On these Stone Altars, I want you to pour on each Altar one pint of the best olive oil you can buy at the local store. When I received the above Prophecy, I prayed to the Lord for a confirmation because I did not have the money for such a trip. Then within two days someone who I had never heard of sent enough money to make the Anointing trip. After receiving the confirmation, I decided to leave on May16. I discussed the trip with Ron Viessman and asked him if he wanted to go, but he had some class exams the following week. After discussing the trip farther, we came up with the idea of having Ron follow me to Mt. Shasta on Friday, and have him return by Sunday, in this way we could use his Jeep on the dirt mountain roads around Mt. Shasta, after the Anointing the Altars. For we both knew my car was not able to get through the mountains roads to the locations that the Lord wanted Anointed. We began to prepare and left at 1:00 PM. on Friday May 16. As with the other such trips the spiritual warfare began to increase. Even now, for several days I have been trying to type this material for the Prophecy Book, and the spiritual warfare has really increased. I wonder if Christians really know this type of spiritual warfare. For I have never heard of it taught or mentioned in churches. It seems all I ever hear in churches is your going to be blessed, your going to be blessed, but never about the reality of Satan and his forces. Oh well, lets move on. Mt. Lassen Altar Anointed on 16 May 1997 about 4:30 PM When we arrived at Mt. Lassen, we found the Park road up to the Mountain closed due to snow, but the area that the Lord wanted an Anointed Altar built was open. So we collected the first stones for the first Altar and Anointed it and prayed at the site, and left for Mt. Shasta. Mt. Shasta South Altar Anointed on 17 May 1997 at 1:00 PM When we arrived in Mt. Shasta City we parked my car and left in Ron's Jeep, and purchased the Anointing Oil at a local store and proceeded toward the dirt mountain road (logging road). Once we arrived at the first Mt. Shasta location (South side), we had Communion and Anointed each other with oil. Then we built the Altar to the Lord out of the local stones, and Anointed it with the olive oil. For some reason I was led to photograph the Anointing Altars. As we had expected the logging road was very bad. In some areas the Jeep almost could not go through for the road was very narrow. At one point we had to build a rock bridge to cross this stream of water to get to the second location on the East side.
This rock bridge took us about 2 1/2 hours to build. We needed it to get to the other side to build the Eastern Altar.
Mt. Shasta East Altar Anointed on 17 May 1997 at 4:00 PM It took us about 2 1/2 hours to build the rock bridge and another half an hour to get to the second location. It did cross my mind several times. "What in the world are we doing out here?" We were pretty tired after building the rock bridge, but we built and Anointed the second Altar to the Lord on the East side of Mt. Shasta. I photographed it 6 days later on my return trip home for I had run out of film after I had photographed the first Altar on the South side of Mt. Shasta. Mt. Shasta North Altar Anointed on 17 May 1997 at 5:00 PM. We found the third site a sandy road off of highway 97. We searched for stones and built the Altar on the North side of Mt. Shasta as we had done the other two sites with an opening on the top to hold the upside down bottle of Olive Oil. But at this Northern Altar the Lord instructed me to make a 6 foot Cross in the dirt in front of the Altar extending North. So I carved a large 6 foot dirt Cross with my shoe on the ground surface extending North. Then the Lord instructed me to walk around the Cross and the Altar Three Times. So we started to walk around the Altar and Cross in a counter clockwise direction, and the Lord stopped us, and told us to walk around the Altar and Cross in a clockwise direction. After we had walked around the Altar and dirt Cross Three Times, the Lord said, "The Cross represents the Hammer that was going to be used to nail the coffin of Satan." Then the Lord instructed me to take the bottle of Wine that we had purchased for Communion and to pour it over the image of the Cross. So I pour the whole bottle of Wine over the image of the 6 foot Cross. Then the Lord said, "The Wine represents the Seal of the Lord." Then Ron took me back to my car and he went home, and I proceeded to Anoint Crater Lake and Mount Saint Helens as per the Lord's instructions. Since now I was in my car with some photographic film, and on the way to Crater Lake, I returned to at the Northern side Altar, and photographed the Altar and Cross. For it was close and just off of Highway 97.
Here is my first camp site was Lake Juanitia. I stayed here when I was going to Crater Lake and when I drove home from Mt. Hood.
Crater Lake Altar Anointed on 18 May 1997 at 3:10 PM. (Sunday) When I arrived at Crater Lake, I found most of it under snow. This made it harder for me because I could not find any stones, and wherever the ground was showing there were people everywhere. But I finally found a place and built an Altar and Anointed it next to the road. This Altar was much smaller, but I Anointed it in the same manner, in the Name of the Father, and of the Son, and of the Holy Spirit. This spot that I found was on the top rim of Crater Lake. The next stop was my sister's house for a stay over and prayer for direction for the other locations or Mountains. 19 May 1997 (Monday) On Monday the Lord instructed me to go to Mount Saint Helens. I arrived at Mount Saint Helens late so I camped there for the night.
I camped at Seaquest State Campgrounds going to Mount Saint Helens, and on the way back from Mt. Rainier.
20 May 1997 (Tuesday) In the early morning hours before the sun came up, the Lord SURPRISED me, and woke me up. He told me to fill my air mattress with air. (I hadn't been blowing up the air mattress, and only using it to lay my sleeping bag on it, to keep any water out that might come under my tent.) During this communication with Lord, the Lord wrote in the Spirit the name "HOOD" in capital letters, which told me to go and build an Altar at Mt. Hood. Then He wrote the letters "OK" over the words "Mt. Rainier." So now I knew, I had to go to Mt. Hood and Mt. Rainier after I Anointed the Altar at Mt. Saint Helens. This information was good because I was planning on going home after Mt. Saint Helens. You have no idea, how hard it was for me to get my tired body out of that warm sleeping bag, and blow air into that air mattress that night, but I did it. Then I tried to get some sleep, and wondered why the Lord wanted my air mattress filled with air. I might add here, that the Lord did frighten me little for I was in a dead sleep state when He awoke me. For after replacing the front brake shoes on my car in front of my sister house that morning, and driving straight for about 5 hours, I did not expect to be awakened in the early morning hours. I'll never understand the "why" of some of these things. Mt. Saint Helens Altar Anointed on May 20 at 12:30 PM. At Mt. Saint Helens, I was not allowed to get any closer to the mountain than the distance we were from Altars we built around on Mt. Shasta. I hiked about .8 of mile along a trail next to a cliff facing the side of where Mt. Saint Helens blew up. I Anointed the Altar at Mt. Saint Helens at 12:30 PM and photographed the site. All of these photographs will be placed on the web site soon, I hope. Mt. Rainier Altar Anointed at 4:55 PM. I Anointed the Altar at Mt. Rainier high on the Volcano's southern side. I had a hard time here too finding some clear ground without snow, but I found a spot near the road. Mt. Hood Altar Anointed on 21 May 1997 at 1:54 PM. At Mt. Hood the ground was also covered with snow, and I had a hard time finding clear ground with some stones for the Altar, but I found a large rock over hanging a cliff off the road. So I carefully climbed on to it, and built and Anointed the Altar there. I had to be very careful for this cliff went down hundreds of feet. But over this large hanging rock the Altar was built, and I headed for home. I was also hoping to back track for 2 hours and stop long enough to photograph the Eastern Altar at Mt. Shasta, the only Altar I had not photographed because I had run out of film. I was frightened of this because it was suppose to rain that afternoon, and I didn't have Ron's Jeep. If I got caught on those dirt logging roads during a rain, I wouldn't be able to get out until the muddy roads dried out. For no one else would be able to use the roads either. But I figured, I could get in and out in 2 hours if I didn't get lost, and getting from that side of Mt. Shasta the roads were a little better. Well two times, I almost decided to return and try to find the Highway 97 for thought I was lost, and the weather looked pretty bad. But I kept praying and praying to the Lord to help me, and He did so. I photographed the Eastern Altar and headed out for home. Praise you Lord!!! I kept wondering while I traveled across California, Oregon, and Washington, why did the Lord need me to Anoint these places in the first place? And the only answer that even came close was, "He told me too, so I had to do it." Who really knows the Mind of God. (over)
|
1050.
Matukio aliyopewa Raymond Aguilera tarehe 16 Mai 1997. Kutoka Unabii #1046 Reymundo, Mimi nataka wewe uende kule kwenye Mlima Shasta na unijengee Madhabahu Matatu ya Mawe pale. Mmoja upande wa kaskazini, mmoja upande wa mashariki, na nyingine upande wa kusini. Kwenye Madhabahu hayo ya Mawe, Mimi nataka wewe ukamimine kwenye kila mmoja wao painti mmoja ya mafuta mazuri sana ya mizeituni ambayo unaweza kuyanunua kwenye duka lolote kwenye eneo hilo. Wakati nilipopokea Unabii huo, Mimi nilimwomba Baba anipe udhibitisho wa agizo hilo; kwa sababu sikuwa na fedha ya kuniwezesha kufanya safari hiyo. Kisha baada ya siku mbili hivi mtu fulani ambaye nilikuwa simfahamu au hata kumsikia alinitumia fedha za kutosha kwa ajili ya safari hiyo ya kwenda kuweka Wakfu maeneo hayo. Baada ya kupokea udhibitisho huo, Mimi niliamua kuanza safari hiyo tarehe 6 Mai. Mimi na Ron Viessman tulijadiliana kuhusu mpango wa safari hiyo; na kumwuliza kama yeye angependa kuungana nami katika safari, lakini yeye aliniambia kuwa alikuwa na mtihani wake fulani katika wiki hiyo inayo kuja. Baada ya kujadiliana naye kwa kina kuhusu safari hiyo, tukakubaliana kuwa Ron anifuate na anikute pale kwenye Mlima Shasta siku ya Ijumaa, na kurudi siku ya Jumapili, kwa njia hiyo tungeliweza kutumia gari lake kwenye barabara ile ya changarawe kuzunguka Mlima Shasta, wakati wa wa kuweka Wakfu Madhabahu ya pale. Kwa maana wote tulijua kuwa gari langu lisingeliweza kuhimili barabara ya kwenye eneo hilo mpaka kufika kwenye eneo lile ambalo Bwana ametuagiza tukapaweke Wakfu. Sisi tulianza matayarisho na kuondoka saa 7:00 mchana ya siku ya Ijumaa tarehe 16 Mai. Kama ilivyokuwa kawaida kwa safari za awali za namna hiyo zilizotangulia, mapambano ya kiroho yalianza kuongezeka. Hata hivi sasa, kwa muda mrefu nimekuwa nikijaribu kuandika ripoti ya safari hiyo kwa ajili ya kuweka kwenye Kitabu cha Unabii bila ya mafanikio kwa sababu mapambano ya kiroho yamekuwa yakiongezeka sana. Kwa kweli najaribu kuwaza kama Wakristo kweli wanajua mapambano ya kiroho ya aina hii. Kwa maana mimi sijawahi kusikia ikiwa inafundishwa au hata angalau kutajwa makanisani. Inaonekana yote ninayosikia makanisani ni kuwa wewe utabarikiwa, wewe utabarikiwa, lakini bila kuelezwa uhalisi wa shetani na majeshi yake. Naam ebu labda tuendelee na shughuli tuliyo nayo. Mlima Lassen Madhabahu yake yaliwekwa Wakfu tarehe 16 Mai 1997 kiasi kama cha saa 10:30 jioni. Pale tulipowasili kwenye eneo la Mlima Lassen, tuligundua kuwa barabara ya kwenda juu kwenye hifadhi ya mlima huo; ilikuwa imefungwa kutokana na theluji, lakini eneo lile ambalo Bwana alitaka tukajenge Madhabahu ilikuwa iko wazi. Kwahiyo sisi tulianza kukusanya mawe kwa ajili ya Madhabahu ya kwanza na kuyaweka Wakfu na kuomba pale kwenye eneo hilo, na kisha tukaondoka kwenda kwenye Mlima Shasta. Mlima Shasta Madhabahu ya Kusini Iliwekwa Wakfu tarehe 17 May 1997 saa 7:00 mchana. Tulipo wasili kwenye eneo la kuegeshea magari kwenye Jiji la Mlima Shasta sisi tuliegesha gari langu na kuliacha pale na kuendelea na safari kwa gari la Ron ambayo ni ya aina ya jipu (kama landrova), na kisha tukanunua mafuta ya mizeituni ya kuweka Wakfu kutoka kwenye duka la hapo na kuendelea kwenye barabara ile ya matope. Mara tulipofika kwenye Mlima ule wa kwanza uitwao Mlima Shasta (upande wa kusini), sisi tulipokea Komunio na kisha tukajiweka sisi wenyewe Wakfu kwa kujipaka mafuta. Kisha tukamjengea Bwana Madhabahu kwa mawe ya maeneo hayo na kuyaweka Wakfu kwa mafuta yale ya mizeituni. Kwa sababu ambayo mimi sielewi niliongozwa kupiga picha yale madhabahu tuliyoyaweka Wakfu. Kama tulivyo tarajia barabara ile ya changarawe ilikuwa ni mbaya kweli. Kwenye maeneo fulani fulani lile gari letu la aina ya jipu; lilikuwa linashindwa hata kupita humo; kwa vile lilikuwa ni nyembamba sana. Sehemu fulani ilibidi tutengeneze kivuko cha mawe ili gari letu hilo liweze kupita kwenye kijito fulani chenye maji na kwenda upande wa pili ili kwenda kwenye eneo la pili lililokuwa upande wa Mashariki.
Kivuko hicho cha mawe kilichukua muda wa masaa 2 1/2 hivi kuijenga. Kivuko hicho ni kwa ajili ya kuvuka upande wa pili kwa ajili ya kujenga Altare ya pili ya Upande wa Mashariki.
Mlima Shasta Madhabahu ya Mashariki Iliwekwa Wakfu tarehe 17 Mai 1997 saa 10:00 jioni Ilituchukua kiasi cha masaa 2 1/2 kulijenga kivuko hicho na masaa mawili kufika kwenye lile eneo la pili. Nilishikwa na maswali kwenye akili yangu na kujiuliza mara nyingi kuwa, "Hivi ni nini hasa tunachokitafuta kwenye maeneo kama haya?" Sisi tulikuwa tumekwisha kuchoka baada ya kujenga kivuko kile cha mawe, lakini sisi tuliendelea na tukamjengea Bwana Madhabahu ya pili ya kwenye eneo la Mashariki ya Mlima Shasta. Kisha mimi nikapiga picha za eneo hilo kwenye safari ya pili siku sita Baadaye, wakati nilipokuwa ninasafiri kurudi nyumbani kwa maana wakati ule tulipojenga madhabahu hayo, mimi nilikuwa nimeishiwa na filamu ya kupiga picha ambayo ili isha kwenye kupiga picha yale Madhabahu ya kwanza kwenye eneo la kusini la Mlima Shasta. Mlima Shasta Madhabahu ya Kaskazini Iliwekwa Wakfu tarehe 17 Mai 1997 saa 11:00 jioni. Tulipata sehemu ya tatu ya kujengea Madhabahu kwenye barabra ya mchanga pembeni mwa barabara kuu Na. 97. Baada ya kupata eneo hilo; tukaanza kutafuta mawe ya kujengea Madghabahu hayo ambayo tuliyajenga kwenye upande wa kaskazini mwa Mlima Shasta, na kama tulivyofanya kwa maeneo yale mengine mawili; tulitengeneza sehemu ya kushikia chupa ya mafuta ya mizeituni. Lakini katika eneo hili la Madhabahu ya Kaskazini Bwana alituagiza tuchore msalaba wenye urefu wa futi 6 ardhini; kuanzia kwenye Madhabahu hayo kuelekea Kaskazini. Kwahiyo mimi kwa kutumia kiatu changu nilichora msalaba mkubwa wenye urefu wa futi 6 ardhini kuelekea Kaskazini. Kisha Bwana akaniagiza kuuzunguka Msalaba huo pamoja na Madhabahu hayo mara Tatu. Kwahiyo sisi tulianza kuuzunguka msalaba huo ulio kuwa umechorwa ardhini pamoja na Madhabahu hayo kwa kuelekea kinyume cha mwendo wa saa na mara Bwana akatusimamisha na kutuambia tuyazunguke Madhabahu hayo pamoja na msalaba ule kwa kuelekea mzunguko wa saa. Baada ya kuuzunguka msalaba huo ulio chorwa ardhini pamoja na Madhabahu hayo mara tatu; Bwana akasema, “Msalaba huo unawakilisha Nyundo ile ambayo inaenda kutumika kupigilia na kufunga jeneza la shetani.” Kisha Bwana aliniagiza kuchukua chupa ile ya Mvinyo tulioununa kwa ajili ya Kumunio na kuimimina juu ya ishara ile ya Msalaba wenye urefu wa futi sita uliochorwa juu ya ardhi. Kisha Bwana akasema, "Mvinyo huo unaashiria Muhuri au lakishi ya Bwana." Kisha Ron alinichukua hadi pale tulipoliacha gari langu; naye akaondoka kurudi nyumbani, nami ninkaelekea kwenda kuweka Wakfu eneo lile la ziwa lililoko kwenye bonde la kreta iitwayo “Crater Lake” pamoja na Mlima wa Saint Helens kama Bwana alivyo agiza. Sasa kwa vile nimerudi kwenye gari langu na nina filamu za kupiga picha, na huku nikiwa ninaelekea kwenye eneo lile la Crater Lake, mimi nikapitia tena kwenye eneo lile ambako tuliweka Madhabahu ya Kaskazini Wakafu ili nikapiga picha Madhabahu yale pamoja na Msalaba ule wa pale ardhini. Kwa sababu palikuwa pako njiani na pale pembeni mwa Barabara Kuu No. 97.
Hapo palikuwa ni eneo la kambi yangu ya kwanza kwenye Ziwa lile liitwalo Juanitia. Nilikaa hapo wakati nilipokuwa ninaenda kwenye ziwa lile la kreta iitwayo “Crater Lake” na tena wakati nilipokuwa ninarudi nyumbani nikiwa nimetokea kwenye Mlima Hood.
Madhabahu ya Kreta Lake Yaliwekwa Wakfu tarehe 18 Mai 1997, saa 9:10 mchana. (Jumapili) Nilipofika pale kwenye ziwa lile lililoko kwenye kreta liitwayo Crater Lake, nilikuta sehemu yake kubwa imefunikwa na theluji. Hali hiyo ilinipa shida kwa sababu ilikuwa vigumu kupata mawe ya kujengea Madhabahu, kila mahali palipokuwa hapajafunikwa na theluji watu walikuwa wamejazana hapo. Baada ya muda kidogo hata hivyo nilipata sehemu iliyokuwa wazi panapofaa kujengea Madhabahu karibu na barabara, nami nikajenga Madhabahu hayo na kuyaweka Wakfu. Madhabahu haya yalikuwa madogo kidogo, lakini mimi nilyaiweka Wakfu kwa namna ile ile, katika Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Sehemu hiyo niliyoipata ilikuwa juu ya ukingo wa Ziwa hilo la kreta. Sehemu iliyofuata ambako nilisimama ilikuwa kwenye nyumba ya dada yangu kwa ajili ya kupumzika na maombi ili kujua maeneo mengine au milima mingine ya kuwekewa wakfu. Tarehe 19 Mai 1997 (Jumatatu) Siku ya Jumatatu; Bwana aliniagiza kuwa niende kwenye Mlima Saint Helens. Mimi nilifika kwenye eneo la Mlima wa Saint Helens jioni kwa hiyo nikapiga kambi yangu kwa ajili ya usiku ule na kulala hapo.
Nilipiga kambi yangu kwenye eneo la kupigia kambi la Seaquest State Campgrounds; wakati nikiwa ninaelekea kwenye Mlima wa Saint Helens, na wakati nimerudi kutoka kwenye safari ya kuweka Wakfu Mlima wa Rainier.
Tarehe 20 Mai 1997 (Jumanne) Asubuhi na mapema ya siku hiyo; kabla jua halija chomoza, Bwana ALINISHUTA kwa kuniamsha. Aliniambia kuwa niende nikaja hewa godoro langu (la hewa). (Mimi nilikuwa sijawahi kulijaza godoro langu hilo kwenye safari hiyo na nilikuwa ninaitumia kama mkeka na kuweka mfuko wangu wa kulalia juu yake ili kuzuia unyevu wowote wa chini ya hema langu usije ukaingia kwenye mfuko wangu huo wa kulalia.) Wakati huo wa mawasiliano na Bwana, Bwana aliandika katika roho yangu neno "HOOD" kwa herufi kubwa, ambayo iliniashiria kuwa niende nikajenge Madhabahu kwenye Mlima Hood. Kisha akaandika herufi "OK" (sawa) juu ya maneno "Mlima Rainier." Kwa hiyo mimi nilijua kuwa inanilazimu kwenda kwenye Mlima Hood na Mlima Rainier baada ya kujenga na kuweka madhabahu ya Mlima Saint Helens. Habari hii ilikuwa ni nzuri kwa sababu mimi nilikuwa nimepanga niende nyumbani baada ya kumaliza kuweka Wakfu Madhabahu ya Mlima Saint Helens. Najua hamjui jinsi ilivyokuwa vigumu kuutoa mwili wangu uliokuwa umechoka kutoka kwenye mfuko wangu ule wa kulalia ambao ulikuwa na joto safi; na kuanza kazi ya kuijaza hewa godoro langu lile la hewa alfajiri ile, lakini hatimaye nilifanikiwa kufanya hivyo. Kisha nikajaribu kupata usingizi kidogo, na kuanza kuwaza ni kwa nini Bwana alitaka nikajaze godoro langu hewa. Labda niongezee hapa kuwa Bwana alinitisha kidogo kwa maana mimi wakati huo nilikuwa kwenye usingizi wa fofo pale aliponiamsha. Kwa maana baada ya kubadilisha breki za mbele za gari langu pale mbele ya nyumba ya dada yangu usiku wa manane wa siku ile iliyopita; na kuendesha kwa masaa matano, mimi sikutarajia kuwa ningeliamshwa mapema kiasi kile. Kwa kweli mimi siwezi kuelewa “Njia na namna” ya mambo hayo. Mlima wa Saint Helens Madhabahu yake yaliwekwa Wakfu tarehe 20 Mai saa 6:30 mchana. Pale juu ya Mlima wa Saint Helens, mimi sikuruhusiwa kwenda karibu na Mlima zaidi ya usawa uliokuwa unafanana na ule wa maeneo yale tulipojenga Madhabahu kwenye mlima Shasta. Mimi nilitembea kwa mwendo wa maili 8 kuzunguka kwa kutumia kinjia cha miguu kuelekea kwenye usawa wa eneo lile ambako Mlima huo wa Saint Helena ulipo lipuka. Nami nikajenga na kuweka Wakfu Madhabahu hayo saa 6:30 mchana na kupiga picha za sehemu hiyo. Picha hizo zote zitawekwa kwenye mtandao siku za hivi karibuni natumaini. Mlima Rainier Madhabahu yake yaliwekwa Wakfu saa 10:55 jioni. Mimi niliweka Wakfu eneo la juu la kusini la kwenye volcano ya Mlima Rainier. Mimi nilipata shida ya kupata eneo lililokuwa ambalo halina theluji, lakini baadaye niliipata karibu na barabara. Madhabahu ya Mlima Hood yaliwekwa Wakfu tarehe 21 Mai saa 7:54 mchana. Pale kwenye Mlima Hood ardhi nayo ilikuwa imefunikwa kwa theluji, mimi nilipata shida ya kupata mawe kwa ajili ya kujengea madhabahu pamoja na kupata sehemu ya ardhi ambayo haikufunikwa kwa theluji, lakini kwa bahati mimi nikapata mwamba fulani ambao ulikuwa unaelekea kwenye bonde pale karibu na barabara. Kwa hiyo mimi nikakwea juu yake kwa umakini na kujenga Madhabahu pale juu yake na kisha nikayaweka Wakfu madhabahu hayo. Ilinibidi niwe mwangalifu sana kwa maana mwamba huo ulikuwa kwenye ukingo wa korongo iliyokuwa inaenda kwa mamia ya futi kwenda chini. Lakini juu ya mamba huo nilijenga Madhabahu, nami nilipomaliza kazi hiyo nikaanza safari ya kurudi nyumbani. Mimi pia nilikuwa natumaini kuwa ningeliweza kurudia njia ile tuliyoipitia hapo nyuma kwa masaa 2 na kusimama kwenye eneo ambalo naweza kupiga picha ya Madhabahu ya Mashariki ya kwenye Mlima Shasta, Madhabahu pekee ambayo sikuweza kufanikiwa kuyapiga picha kwa vile mimi kwa wakati huo nilikuwa nimeishiwa na filamu ya picha. Mimi nilikuwa nimetishwa na wazo hilo kwa sababu ilikuwa imetabiriwa na wataalamu wa hali ya hewa kuwa ingeliyeshe mchana ule; nami sikuwa na gari lile la aina ya jipu ya Ron. Hivyo kama nitakwama kwenye barabara ile ya matope wakati wa mvua najua kwa uhakika nisingeliweza kutoka mpaka barabara hiyo ya matope ikauke. Kwani mimi nilikuwa sitarajii kama kuna mtu mwingine ambaye anaweza kuitumia barabara hiyo kwa wakati huo. Lakini mimi nikadhani kuwa ningeliweza kuingia na kutoka katika muda wa masaa 2 kama sitapotea njia, na kuanzia upande ule wa Mlima Shasta barabara ilikuwa afadhali kidogo. Naam mara mbili mimi kidogo niamue kurudi ili kutafuta Barabara Kuu Na. 97 kwa maana mimi nilidhania kuwa labda nimekwisha potea njia, na hali ya hewa ilikuwa inaonekana kama inataka kuchafuka. Lakini mimi niliendelea kumwomba Bwana ili anisaidie, Naye alinisaiidia kweli. Nilifanikiwa kupiga picha ya eneo hilo la Madhabahu ya Mashariki na kisha nikaendelea na safari yangu ya kurudi nyumbani. Usifiwe Ee Bwana!!! Mimi nikawa na mawazo akilini kwangu wakati nilipokuwa safarini kupitia majimbo ya Kalifornia, Oregon, hadi Washington, nikiwa ninajiuliza kwanza ya yote; ni kwa sababu gani Bwana alinitaka mimi kuweka maeneo hayo Wakfu? Lakini jibu pekee lililokuwa linanijia kwenye akili yangu ambalo linakaribiana na ukweli ni kuwa “Naam Yeye ndiye aliyeniambia hayo kwa hiyo ilikuwa inanilazimu kufanyia hivyo.” Hivi ni nani ajuaye kwa uhakika Mawazo ya Mungu. (Mwisho). |
e-mail:Ray@prophecy.org
Kusaidia huduma hii Bonyeza
hapa.
au andika kwa: Raymond Aguilera, S.L.P.20517, El Sobrante, CA. 94820-0517, USA.
Kuagiza Vitabu vya Unabii bonyeza
kwenye kitabu 
Haki ya kunakili © 1989-2001, Raymond Aguilera, Prophecy.org (sm) Haki zote zimehifadhiw
Kurudi Kwenye Jalada la Kitabu cha Unabii.
Kurudi Kwenye Orodha ya Yaliyomo. (1-1000)
Kurudi kwenye Orodha ya Yaliyomo 2 (1000 + )