|
869.
Prophecies and Visions given to Raymond Aguilera on 5 March 1996 at 8:00 PM. Note: These visions and prophecies were received during worship (except for the last seven) at our weekly Tuesday night communion and prayer meeting- that some nine men and women gather. Almost from the start of the worship music, I found myself face down and flat on the floor, with my hands out in the form of a "T", and weeping from the events that I saw during the two hours on the floor. Vision: Before my face went to the floor, I saw a large red check mark over the projected song that was on the wall. (over) Vision: Then I had a vision of a large cloud covered Planet that I saw back in # 2 Prophecy on 18 July 1990, but this time it looked small and was being held between the Lord's thumb and first finger. Vision: As I watched- I saw a black string wrapped around the Finger of the Lord and the Finger was pulled up with a string. I could see the clouded planet left on top of the Thumb. Then the Thumb was removed, and the planet was left alone in outer space. Vision: Then I saw the Lord's whole Hand- but in a Fist, with the string still tied to the first Finger. Then I saw a black string tied around the Wrist and the string was pulled and the whole Arm lifted up to the vertical position. (over) Vision: The next vision was a sensor like the kind the Lord speaks about in the bible, and someone was placing incenses in it- to burn. But before the contents were burned I saw something that looked like snow flakes falling from the air onto the sensor. So much of the white stuff fell on top of the sensor and the surrounding area - that a mound about 10 feet high covered the sensor, and the sensor could not be seen anymore. Then this white stuff changed into a gold looking mound that started to radiate or glow with a white cloud look. As this mound was radiating; this round rainbow appeared in mid-air about half way up the glowing clouds. Prophecy: I asked myself, "What is this stuff." The Lord said, "Those are the prayers of the saints." (over) Vision: Then I saw the Bride of Christ standing in front of the Lord, but with her back facing the Lord, and the Lord had His Arms around her. They Both were - just standing there quietly - and swaying from side to side. Then this large white glowing ring that looked like a Hula-Hoop appeared around them and it started to sway and rock up and down around them. The ring had more of a teeter-totter movement. (over) Vision: Then out of nowhere a large nuclear explosion appeared and quickly disappeared. (over) Vision: As I was in the spirit and wondering what had just happened, I noticed a man dancing to the worship music in the spirit and wondering who he was. Then I heard a voice say, "It's Me, Jesus." I stood watching Jesus dance in perfect time to the worship music. Then He motioned me to come down, and dance with Him. All that came to my mind was my sinful nature, all of my past unbelief, and I felt so unworthy. All these things were running through my mind as He beckoned me down. How could He asked me to dance with Him with all of my doubts. So I went down and stood beside Him and He took my right hand with His Left Hand. We were standing like in a line dance or how Greek men dance side-by-side. At first, I tried, but this feeling of unworthiness was all over my physical body, as I was viewing it in the spirit, and I began to cry and cry in the flesh with my face flat on the floor. And I told Jesus, "I can't do this! I'll just watch you dance." So I stood back and watched Him dance and dance and dance to the uplifting worship music with perfect timing. Then He motioned me again, and said, "Come- and try it again just follow Me. It's easy." So I gave it another try and before long we were dancing side-by-side all over the place in perfect timing to the worship music. One other thing, I became so overwhelmed in the flesh that I cried, but I danced in the spirit with such joy; I became high with happiness, in the flesh and in the spirit, once I learned how to follow the Lord. It got to the point where I was so happy in dancing, that Jesus stepped back and watched me dance for Him. I was so happy that I didn't want to ever stop. Vision: Then the vision changed and I saw four grave stones dancing to the same worship music. It looked funny at first, but they kept perfect time to the music too. So I took a second look, but this time each grave stone had a left arm and they were all holding a large spoon almost as large as the grave stone itself; as they danced in perfect timing swings and waving their large spoons in the air. Unusual looking, but very real. Vision: All of sudden the vision changed again, but this time I saw a mid-eastern looking man dancing to the music. Then a man wearing a suit; then a woman, and before long there were people dancing as far as the eye could see. Millions and millions of people - all dancing with perfect timing to the worship music. It was INCREDIBLE watching it in the spirit; this mass of humanity moving without one person missing a step to the FAST uplifting worship music. Like I said earlier it was like line dancing. All the people were dancing side-side and facing forward. Vision: The next vision was of a judge's mallet coming down as the people danced in perfect form to the FAST worship music; as the Lord watched. As I watched the mallet come down and hit the wooden plate, I thought for sure I would see someone fall out of step or disappear. But nothing happened and the people kept on dancing as if they didn't even hear the judge's mallet come down. This happened three times, but not one person missed a step. Note: It seems unusual as I type this - for I can almost hear and feel the fast worship music, and see all of those people dancing in rhythm before the Lord. It seemed the Lord was saying- that anyone who is in step with Him doesn't have to worry about judgment. They don't even hear it, because they are in Him and with Him, and in His protection. Vision: The next vision was of Jesus Christ dancing alone with the Bride of Christ. They had the whole dance floor to themselves for I couldn't see anyone else there. They reminded me of Fred Astaire and Ginger Rogers swinging and twirling around and around in this vast open space, in perfect timing to the worship music. I could see the Bride wearing on Her head, this large wide white hat with this black ribbon around the hat. I looked a second time, and this time She was wearing a different large hat (same style), but with light colored ribbons (yellow & white) coming out of the top of the hat. The third hat was also large and white, but it looked like it had holes around the brim almost as if it was crocheted. But the most interesting thing was their movement. They were always in PERFECT TIME to the music. Note: This was one of the BEST visions in the spirit I have ever had and will remember it for many years. (over) Vision: Then after worship and during the prayer time, I saw a liquid silver metal looking man beginning to play golf. The man reminded me of the Terminator in the movie Terminator 2 that moved like liquid metal. While watching him take this small round ball and place it on the ground. I began to wonder who he was. Prophecy: Then I heard a voice say, "It's Me, Jesus!" I said, "JESUS- do you play golf!" with a surprised sound coming out of my spirit. And Jesus said, "I'm going to HIT that BALL into that HOLE!" (over) Vision: Then the next vision was of a man wearing a pair of dark sun glasses; the kind that the Secret Service wear when they protect the President of the United States. (over) Vision: The next vision was of a Dove flying and staying in mid-air with slow moving wings; like what a humming bird would do, but the wings were moving slowly. Then the vision changed and a glass of water appeared in front of the Dove and the Dove began to drink the water. (over) Vision: The next vision was of a vulture's head. (over) Vision and Prophecy: The next image was of a beautiful little bird saying to the Lord, "Heal my throat for I cannot sing." Then the Lord said to the little bird, "Open your beak and let Me see inside your throat." After looking inside the little bird's throat, I saw the Lord move back as the little bird closed its beak. And the Lord said, "Move on - there is nothing wrong with your throat!" (over) Vision: Somehow after this, I found myself in the spirit, but way-out in outer space. As I looked down at the stars I could see that they had a slow swirling motion. (over)
|
869. Unabii
na Maono aliyopewa Raymond Aguilera tarehe 5 Machi 1996, saa 2:00 usiku. Angalizo: Maono hayo na unabii yaliyo pokelewa wakati wa maombi (isipokuwa zile saba za mwisho) kwenye mkusanyiko wa maombi na kushiriki Komunio (chakula cha Bwana) ya kila Jumanne ya wiki ya wanaume na wanawake tisa. Karibia toka kuanzia mwanzo wa nyimbo, mimi nilijikuta nikiwa nimelala sakafuni uso chini na huku nikiwa nimepeleka mikono yangu ambayo iliunda herufi "T", na huku nikiwa nalia kutokana na yale matukio niliyo kuwa ninayaona wakati wa masaa yale mawili nikiwa pale sakafuni. Maono: Kabla uso wangu haujaenda sakafuni, mimi niliona maono ya alama kubwa ya vema juu ya wimbo uliokuwa umeandikwa ukutani. (Mwisho). Maono: Kisha niliona maono ya sayari fulani kubwa sana iliyofunikwa na mawingu ambayo niliwahi kuiona hapo kwenye unabii # 2 ya tarehe 18 Julai 1990, lakini safari hii ilikuwa ni ndogo ikiwa imeshikiliwa katikati ya Kidole Gumba na Kidole cha kwanza cha Mkono wa Bwana. Maono: Nilivyo kuwa na angalia niliona uzi mweusi ukiwa umesokotwa kwenye Kidole cha Bwana, na Kidole hicho kikavutwa kwenda juu pamoja na kamba hiyo. Mimi nilikuwa naweza kuona sayari hiyo ilitoka juu ya Kidole Gumba cha Bwana. Kisha Kidole Gumba hicho kikaondolewa na sayari hiyo ikaachwa kwenye anga za juu. Maono: Kisha nikaona Mkono wote wa Bwana lakini ukiwa umekunjwa na kuwa Ngumi na uzi ule ukiwa bado umefungwa kwenye Kidole Chake cha Kwanza. Kisha niliona uzi ule mweusi ukiwa umefungwa kwenye kiwiko cha Mkono wa Bwana, na uzi ule ulipovutwa Mkono wote ulinyanyuka wima. (Mwisho). Maono: Maono yaliyofuata yalikuwa ni aina ya chombo cha kuwekea ubani ambacho Bwana alikuwa ameiongelea katika Biblia, na mtu fulani alikuwa anaweka ubani ndani yake ili kuuchoma. Lakini kabla ubani huo haujachomwa mimi niliona kitu kilichokuwa kina fanana na chembe chembe ya barafu ikianguka kutoka angani hadi kwenye chombo hicho. Chembe chembe hizo nyingi za barafu zilianguka kwa wingi ndani ya chombo hicho na kuzunguka eneo hilo kiasi ambacho ilitengeneza rundo kubwa la kiasi cha urefu wa futi 10 juu ya chombo hicho, na chombo hicho kikawa hakionekani tena. Chembe chembe hizo nyeupe mara zilibadilika na kuwa kitu kinacho fanana na rundo la dhahabu. Ambayo ilianza kumeremeta kama wingu nyeupe sana angavu. Wakati rundo hilo lilipokuwa linameremeta; upinde wa mvua mara ukajitokeza katikakati ya anga kiasi cha nusu ya anga juu ya rundo hilo lililokuwa linameremeta. Unabii: Mimi nilijiuliza mwenyewe, "Hii nayo ni vitu gani." Bwana alisema, "Hayo ni maombi ya watakatifu." (Mwisho). Maono: Niliona Bibi Harusi wa Kristo akiwa amesimama mbele ya Bwana, lakini akiwa amemgeuzia Bwana mgongo wake, na Bwana akiwa simama nyuma yake na amemzungushia mikono yake. Nao wote wawili - wakiwa wamesimama tu pale kimya na wakiwa wanayumba upande huu na upande ule. Kisha pete fulani iliyokuwa inameremeta ambayo ilikuwa inaonekana kama Hula-Hoop ikajitokeza katikati yao na ikaanza kupanda juu na chini kuwazunguka wao. Kisha pete hiyo ikaanza kuwa na mzunguko wa teeter-totter. (Mwisho). Maono: Kisha bila ya matarajio mlipuko mkubwa wa kinuklia ulitokea kwa ghafla na kupotea kwa ghafla. (Mwisho). Maono: Wakati nikiwa katika ulimwengu wa kiroho na huku nikiwa na tafakari kile kilochotokea muda mfupi uliopiata, nilimwona mtu aliyekuwa anacheza kufuatia muziki huo wa kuabudu katika ulimwengu wa Kiroho na huku nikiwa na waza ni nani mtu huo. Kisha nikasikia sauti hii, "Ni Mimi Yesu." Nilisimama huku nikiwa ninamwangalia Yesu akiwa anacheza katika hatu safi inayo lingana na muziki huo wa kuabudu. Kisha Akanipungia kuashiria kuwa niende huko, na kucheza pamoja Naye. Yote yale yaliyonijia kwenye mawazo yangu yalikuwa ni hali yangu ya dhambi, kutokuamini kwangu hapo awali nami nikajisikia kuwa sistahili kabisa. Mambo haya yote yalikuwa yakipita kwenye mawazo yangu wakati alipokuwa ananiita mimi. Itawezekananaje yeye kuniita tucheze Naye pamoja, pamoja na mashaka yangu haya yote. Kwa hiyo mimi nikaenda kule chini aliko na kusimama karibu Naye, Naye akachukua mkono wangu wa kulia kwa Mkono Wake wa Kulia. Sisi tulikuwa tumesimama katika mstari ubavu kwa ubavu au kama wanaume wa Kigiriki wanavyo cheza ubavu kwa ubavu. Mwanzoni, nilijaribu, lakini kule kujisikia kuwa sistahili kulinitawala kwenye mwili wangu wote wa nyama, wakati nikiwa ninaangalia hayo yote katika ulimwengu wa kiroho, nami nikaanza kulia na kulia katika mwili nikiwa nimelala kwa uso wangu sakafuni. Nami nikamwambia Yesu, "Mimi siwezi kufanya hivi! Mimi nitakuangalia Wewe ukicheza." Kwa hiyo mimi nisogea nyuma nikiwa namwangalia Yeye akiwa anacheza na kucheza kwa hatua za kufuatiza muziki huo wa kuabudu uliokuwa unanyanyua moyo, kwa uhakika. Kisha akanipungia mimi tena, na kusema, "Njoo na ujaribu ukinifuatisha Mimi. Ni rahisi." Kwa hiyo mimi nikajaribu tena, na kabla muda mrefu haujapita; sisi tulikuwa tunacheza ubavu kwa ubavu sehemu hiyo yote kwa hatua iliyokuwa inaoana na mapigo ya muziki huo wa kuabudu. Kitu kingene ni kuwa mimi nililemewa sana kwenye mwili kiasi ambacho nililia, lakini mimi niliendelea kucheza katika ulimwengu wa kiroho kwa furaha kubwa; na huku nikiwa nimejawa na furaha kubwa sana; katika mwili na katika roho, mara tu nilipojifunza jinsi ya kumfuatia Bwana. Ilifikia mahali ambako mimi nilikuwa na furaha kubwa wakati nikiwa na cheza kiasi ambacho, Yesu akarudi nyuma akawa ananiangalia nikiwa ninamchezea Yeye. Mimi nilikuwa na furaha kubwa kiasi ambacho mimi sikutaka kuacha kucheza dansi hiyo tena. Maono: Kisha maono hayo yakabadilika nami, nikaona mawe ya makaburi manne yakiwa yanacheza kufuatia sauti ya muziki huo wa kuabudu. Ilikuwa inaoneka kama kioja hapo mwanzoni, lakini yaliweka hatua iliyokuwa inaoana vizuri kabisa na muziki huo. Kwa hiyo mimi nakaangalia kwa mara nyingine kwa uangalifu, lakini safari hii kila jiwe la kaburi lilikuwa na mkono wa kushoto na wote walikuwa wameshikilia kijiko kubwa ambacho kilikuwa kikubwa sawasawa na jiwe la kaburi hilo; wakati walipokuwa wanacheza katika hatua iliyokuwa barabara kabisa wakiwa wanapunga vijiko hivyo kutoka hewani. Yalikuwa hayaonekani kama kitu kigeni sana lakini yalikuwa ni mambo halisi sana. Maono: Kwa ghafla maono hayo yakabadilika tena, lakini safari hii mimi nilimwona mtu aliyekuwa na mashariki ya kati akiwa anacheza dansi ya muziki huo. Kisha mtu aliyekuwa amevaa suti; na kisha mwanamke aliyevaa suti, na kabla ya muda mrefu nikaona watu wengi wakiwa wanacheza hadi kwenye mwisho wa upeo wa macho. Mamilioni na mamilioni ya watu wakiwa wanacheza kwa hatua iliyokuwa inalingana vizuri sana na muziku huo wa kuabudu. Ilikuwa ni AJABU SANA kuwaangalia jeshi hilo la bahari ya watu katika roho bila mtu hata mmoja kukosea hatu kwenye muziki huo wa KASI wa kuabudu. Kama nilivyo kwisha kusema hapo awali ilikuwa ni kama wanacheza katika mstari. Watu wote walikuwa wakicheza ubavu kwa ubavu wakiangalia mbele. Maono: Maono yaliyo fuata yalikuwa ni ya nyundo ya hakimu ikakonga wakati watu walipokuwa wanacheza kwa hatua nzuri kwa muziki wa HARAKA HARAKA wa kuabudu; wakati Bwana akiwa anaanglia. Wakati nikiwa ninaangalia nyundo hiyo ikigonga juu ya sahani ya mbao, mimi nikajiwazia kuwa bila shaka mtu mmojawapo atakosea hatua au kupotea. Lakini hakuna lolote lililo tokea na watu waliendelea kucheza kana kwamba wao wala hawakusikia nyundo ile ya hakinu ikigonga. Hii ilijirudia mara tatu, lakini hapakuwa na mtu hata mmoja aliye potea hatu. Angalizo: Inaonekana kama ni kitu cha ajabu ninavyo andika haya kwa maana nikama nasikia na kuhisi muziki huo wa kuabudu, na kuona watu hao wote waliokuwa wanacheza dansi mbele ya Bwana kwa hatua. Inaonekana kama Bwana akisema mtu yeyote anaye fuata Hatua Zangu hana haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu Hukumu. Kwa maana wao hata ile kusikia hawatasikia, kwa sababu wao wako ndani Yake, na wako pamoja Naye, na wako kwenye ulinzi wake. Maono: Maono yaliyofuata yalikuwa ni ya Yesu Kristo akiwa anacheza peke yake na Bibi Arusi wa Kristo. Wao walikuwa wamepewa nafasi yote ya ukumbi huo kwa maana mimi nilikuwa simwoni mtu mwingine Yeyote pale. Walinikumbusha mchezo wa Fred Astaire na Ginger Rogers wanacheza kwa kuyumba kutoka huku hadi kule kwa kuzunguka katika eneo hilo kubwa sana sana, bila kukosea hatua na mdundo wa muziki wa kuabudu. Mimi nilikuwa naweza kumwona Bibi Harusi akiwa amevaa kofia fulani kubwa nyeupe iliyokuwa na utepe kuzunguka kwenye kofia yake. Mimi niliangalia kwa mara ya pili, na wakati huu alikuwa amevaa kofia nyingine kubwa (muundo ule ule), lakini ilikuwa na utepe wa rangi ya uweupe uliofifia (manjaro na nyeupe) ikijitokeza juu ya kofia hiyo. Kofia ya tatu ilikuwa kubwa pia na nyeupe, lakini ilikuwa inaonekana kuwa na matobo kuzunguka mviringo wa kofia hiyo kanakwamba ilikuwa imerembwa. Lakini la kuvutia kushindwa yote ilikuwa ni kule kucheza kwao. Kwa maana wakati wote walikuwa kwenye HATUA SAFI inayoendana na muziki huo. Angalizo: Maono hayo ni moja ya maono MAZURI sana niliyo wahi kuyaona katika roho, na nitayakumbuka kwa miaka mingi ijayo. (Mwisho). Maono: Kisha baada ya kuabudu na wakati wa maombi, niliona mtu aliyekuwa anafanana na yule mtu wa rangi ya maji maji ya chuma ya fedha akianza kucheza mpira wa kupiga kwa gongo (golf). Mtu huyo alinikumbusha yule mtu wa kwenye sinema anayeitwa Terminator kwenye sinema ya Terminator 2 ambaye alikuwa natembea kama chuma ya maji maji. Wakati nilipokuwa namwangalia yeye akichukua mpira huo mdogo na kuuweka juu ya ardhi. Mimi nikaanza kuwaza kuwa huyo mtu alikuwa ni nani. Unabii: Kisha nikasikia sauti ikisema, "Ni Mimi Yesu!" Nikasmea, "YESU hivi unajua kucheza mpira wa magongo!" na sauti ya kushangaa ikiwa inatoka kwenye roho yangu. Yesu akasema, "Mimi naenda KUUTWANGA MPIRA ule hadi kwenye SHIMO!" (Mwisho). Maono: Kisha maono yaliyofuata yalikuwa ni ya mtu aliyevaa miwani nyeusi ya jua ya aina ile inayovaliwa na askari wa Usalama pale wanapomlinda Rais wa Marekani. (Mwisho). Maono: Maono yaliyofuata yalikuwa ni ya Njiwa akiwa anaruka na kukaa angani akiwa anapepesa kidogo sana mabawa yake; kama yule ndege anayetoa sauti ya kuguguna afanyavyo, lakini mabawa yake yalikuwa yanaenda kidogo kidogo. Kisha maono hayo yakabadilika na bilauri ya maji ikajitokeza mbele ya Njiwa huyo na Njiwa huyo akaanza kuyanywa maji hayo. (Mwishoi). Maono: Maono yaliyofuata Yalikuwa ni ya kichwa cha tai. (Mwisho). Maono na Unabii: Maono yaliyofuata yalikuwa ni ya ndege fulani mdogo mzuri; akimwambia Bwana, "Tibu koo langu kwa maana nashindwa kuimba." Kisha Bwana akamwambia yule ndege mdogo, "Ebu fungua mdomo wako ili nipate kuona ndani ya koo lako." Baada ya kuuangalia ndani ya koo la ndege huyo mdogo, nilimwona Bwana akisogea nyuma wakati ndege huyo mdogo alipokuwa anafunga koo lake. Na Bwana akasema, "Endelea - kwa maana hakuna tatizo kwenye koo lako!" (Mwisho). Maono: Kwa namna fulani, mimi nilijikuta niko kwenye ulimwengu wa kiroho, lakini juu sana, kwenye anga za juu. Nilivyo kuwa na angalia chini kwenye nyota, nilikuwa naweza kuona yalikuwa yanazunguka pole pole. (Mwisho).
|
e-mail:Ray@prophecy.org
Kusaidia huduma hii Bonyeza
hapa.
au andika kwa: Raymond Aguilera, S.L.P.20517, El Sobrante, CA. 94820-0517, USA.
Kuagiza Vitabu vya Unabii bonyeza
kwenye kitabu 
Haki ya kunakili © 1989-2001, Raymond Aguilera, Prophecy.org (sm) Haki zote zimehifadhiw
Kurudi Kwenye Jalada la Kitabu cha Unabii.
Kurudi Kwenye Orodha ya Yaliyomo. (1-1000)
Kurudi kwenye Orodha ya Yaliyomo 2 (1000 + )